
HOJA YA ZITTO KABWE NI HII
Moja ya msingi Mkuu wa sera ya mambo ya Nje ya Tanzania Ni kusimama upande wa wanyonge popote walipo duniani. Kutokana Na msingi huu Tanzania imekuwa bega Kwa bega Na watu wa Sahara Magharibi ( POLISARIO ) Na Palestine ( PLO ).
Kumekuwa Na juhudi kubwa ya Mataifa mbalimbali ya Afrika kuondoa utambuzi wake wa Jamhuri ya Sahrawi ( SADR ) hata kufunga Balozi za Nchi hiyo kwenye Nchi hizo za Afrika. Yote haya yanafanywa Kwa msaada mkubwa wa Nchi ya Morocco ambayo inaikalia Kwa mabavu Jamhuri ya Sahrawi.
Morocco imekuwa ikifanya kampeni zake hapa Tanzania Pia. Wanasiasa kadhaa wamekuwa wakikirimiwa na Ufalme wa Morocco na kujaribu mara kadhaa kupenyeza ajenda ya Morocco kwamba Sahara Magharibi Ni sehemu ya Morocco na hivyo Tanzania iondoe kuitambua kwake SADR na kuiondoa kwenye kiti chake Umoja wa Afrika. Habari zilizopo kwenye 'corridors' za kidiplomasia zinaonyesha kuwa Mfalme wa Morocco atakuwa mgeni wa Rais wetu ndani ya Siku chache zijazo.
Wanaohusika Na mipango ya kuvunja msingi Mkuu wa sera ya mambo ya Nje ya Tanzania wakumbuke kwamba UKIJARIBU KUVUNJA MISINGI, UTAVUNJIKA MWENYEWE. Kinachoitwa diplomasia ya kiuchumi kisiwe kichaka cha kuacha mapambano dhidi ya ukoloni, ugandamizwaji Na ubeberu.
Mwalimu Nyerere alituachia heshima ya kuwa Nchi yenye misingi. Siku tunawapa mgongo watu wa Sahara Magharibi, Mwalimu Nyerere atageuka kaburini alipopumzika. Nasi tutakuwa Taifa la hovyo kama Mataifa mengine Afrika ambayo yanauza utu wao Kwa vipande vya sarafu aka Diplomasia ya Uchumi. Tupo ambao hatutakubali Na hatutokaa kimya.
Mwaka 1965 vijana jeuri wa Tanzania waliandamana kupinga UDI licha ya katazo la Serikali ya Mwalimu Nyerere. Sitashangaa hata kidogo kuona UDI ikijirudia mwaka 2016 mbele ziara hiyo ya Mkuu wa Nchi inayokalia Nchi nyengine Kwa mabavu ( occupying power ).
Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi ina Wajibu wa kuwaeleza Watanzania juu ya msimamo wetu kuhusu Sahara Magharibi vinginevyo Serikali isije kulaumu Vijana wenye ujasiri wa kulinda heshima Na msingi wa Nchi yetu - Sera yetu ya Mambo ya Nje inayosimama Na wanyonge.
Comments zikawa hivi
Zungu Mussa Of all the people Zitto you know better .Morocco haikufukuzwa AU walijiondowa wenyewe baada ya Africa kuwapa Kiti Polisario ,hii ni fursa nzuri ya kuwaweka pamoja na kutatuwa matatizo yao tiari kuna azimio la UN la referendum .Tanzania tunajuwa haki za wa Palestine lakini tuna mahusiano na Israel haimanishi tumeachana na msimamo wetu, Leo asilimia kubwa za nchi zilizo pigana na Israel zina mahusiano hasa nchi za Arabuni.Tanzania inanafasi kubwa ya kuzishawishi pande zote mbili kufikia muafaka wa kuingia kwenye kura za maoni kwa azimio la UN
Zitto Kabwe Kuna kampeni kubwa kuwaondoa SADR katika kiti chao AU. Mpaka Sasa wamebakiza Nchi 6 tu kuweza kufikia lengo Lao hilo. Nasikitika sana Nchi yangu inakwenda kuondoa nguvu yake nyuma ya POLISARIO




ConversionConversion